Mrithi wa Maalim Seif ajitokeza

 


Makamu Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Zanzibar, Juma Duni Haji, amejiuzulu nafasi hiyo na ameamua kuchukua maamuzi hayo sababu ana nia ya kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa chama hicho kwa ngazi ya Taifa, baada ya aliyekuwa Mwenyekiti wao Maalim Seif Sharif Hamad kufariki dunia.

Taarifa hiyo imetolewa leo Novemba Mosi, 2021, na Naibu Katibu wa Habari wa chama hicho Janeth Rithe, na kusema kuwa Duni aliandika barua yake ya kujiuzulu nafasi yake ya Makamu Mwenyekiti mnamo Oktoba 30, mwaka huu.


Uchaguzi wa Mwenyekiti wa chama, Makamu Mwenyekiti wa Zanzibar na uchaguzi wa nafasi moja ya Mjumbe wa Halmashauri Kuu Taifa, utafanyika Januari 29, 2022.

Post a Comment

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

Previous Post Next Post