HIVI HAPA VIGONGO VYA YANGA VILIVYOBAKI KABLA YA KUFUNGA HESABU ZA LIGI KUU BARA MSIMU HUU



MABINGWA wa Kihistoria wa Ligi Kuu Bara Tanzania, Yanga kwa sasa wamecheza jumla ya michezo 34 na wamejikusanyia jumla ya pointi 80 kibindoni.

Yanga ina rekodi ya kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu mara nyingi kuliko timu zote ambapo mpaka sasa wametwaa taji hilo mara 27.

Kwenye michezo yao 34 waliyocheza wamepoteza michezo minne tu na kutoa sare michezo mitano na imeshinda jumla ya michezo 25.

Ili kutimiza michezo 38 na kufunga hesabu za Ligi Msimu huu wamebakiza mechi nne na ratiba yake ipo namna hii:-

Mei 9 Biashara United v Yanga, Karume.

Mei 14 Ruvu Shooting v Yanga, Uwanja wa Mabatini.

Mei 22 Yanga v Mbeya City, Uwanja wa Taifa.

Mei 28 Yanga v Azam FC, uwanja wa Taifa.

Post a Comment

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

Previous Post Next Post