Wema kwa mara ya kwanza amesema kuwa hajawahi kukata utumbo ili apungue kama watu wanavyodai, isipokuwa kipindi alichopitia kwenye lile sakata la kuvuja kwa picha zake za chumbani na Patric Christopher ‘PCK’ kilikuwa kigumu mno kwani alikuwa anapitisha hata siku tatu bila kula chochote mpaka anapepesuka.
“Watu nawashangaa sana, wanaona kukatwa utumbo ni kitu rahisi ee? Mimi nimekonda kwa sababu ya mawazo makali niliyokuwa nayo na si vitu vingine maana nilikuwa kwenye wakati mgumu sana", amesema Wema.
Wema ameongeza kuwa, "Yaani hujui tu ninavyoufurahia huu mwili wangu wa sasa, nimekuwa sio mzito tena na navaa nguo ambazo nataka na napendeza zaidi tofauti na ilivyokuwa huko nyuma, kwa kifupi najipenda hivi nilivyo".
Tags
CELEBRITY