Simba Kuwakosa Nyota Wake Hawa Kwenye Mchezo wao na Stend United

 Simba Kuwakosa Nyota Wake Hawa Kwenye Mchezo wao na Stend United
Nyota wa timu ya Simba kiungo mkabaji Jonas Mkude na James Kotei wataukosa mchezo wa kesho dhidi ya  Stand United utakaochezwa kesho uwanja wa Taifa Dar es Salaam.

Mkude ataukosa mchezo huo kutokana na kuendelea kuuguza majeraha  aliyoyapata katika mchezo dhidi ya African Lyon, Kotei akitumikia adhabu ya kufungiwa mechi tatu baada ya kile kilichotafsiriwa  kumpiga ngumi beki wa Yanga Gadiel Michael katika mchezo wao dhidi ya Yanga.

"Kwa sasa naendelea vizuri namshukuru Mungu hivyo nina imani muda si mrefu nitakuwa sawa kwa ajili ya kuendelea kupambania timu yangu na taifa kwa ujumla"alisema Mkude.

Post a Comment

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

Previous Post Next Post