MCHEZAJI HUYU WA LIVERPOOL ATUA BONGO JANA


Tanzania imepokea ugeni, ni mchezaji wa zamani wa Liverpool

Asikwambie mtu Bongo nzuri, inavutia na tamu, kama ulikuwa hujui chukua hii toka kwangu, beki kitasa wa zamani wa Liverpool Martin Skrtel ambaye kwa sasa anakipiga Fenerbahce ameshuka Kilimanjaro International Airport kwa ajili ya kutembelea vivutio mbalimbali nchini.

Taarifa za ujio wake nilizinyapia kupitia account yake ya instagram baada ya ku-post tickets tatu (yeye, mkewame na mtoto) zikionesha wanakuja kutembelea Tanzania.

Mishale ya saa 7:30 usiku jamaa akatua zake nchini pamoja na familia yake.

Post a Comment

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

Previous Post Next Post