JE, Ronald Leo Ataweza Kuonesha Kuwa ni Mbabe wa Kutikisa Nyavu Kombe la Dunia?



Michuano ya Kombe la Dunia nchini Urusi inaendelea tena leo katika viwanja vitatu ambapo nyota wa Ureno Cristiano Ronaldo atakuwa dimbani kuiongoza timu yake ya taifa kukipiga dhidi ya Iran katika mchezo wa Kundi B kwenye uwanja wa Mordovia kuanzia saa 3 kamili usiku. 

Nyota wa Ureno Cristiano Ronaldo aliyenyoosha kidole akiwa na nyota wa England, Harry Kane.

kuelekea mechi hiyo, Ronaldo anapewa nafasi kubwa ya kuonesha ubabe wake wa kutikisa nyavu baada ya kutikisa kamba za wapinzani mara nne katika mechi mbili alizocheza.

Endapo Ronaldo atafunga bao moja dhidi ya Iran atakuwa amemzidi nyota wa England, Harry Kane aliyefikisha mabao matano katika mashindano hayo.

Mechi nyingine zitakazopigwa ni Misri ambao wameshaaga mashindano watakamilisha ratiba dhidi ya Saudi Arabia majira ya saa 11 jioni huku pia Uruguay wakikipiga na wenyeji Urusi muda huohuo wa saa 11.

Post a Comment

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

Previous Post Next Post