IMETHIBITISHWA: Hadi muda huu Wawa bado hajasaini mkataba Simba


Pascal Wawa ameshafanya mazoezi na Simba kwa siku tatu hadi nne tangu arudi nchini huku akihusishwa kujiunga na ‘Wekundu wa Msimbazi’ baada ya kufanya vizuri akiwa na Azam FC kabla hajaondoka Tanzania.

Ishu ni kwamba jamaa bado hajasaini mkataba na mnyama licha ya kuanza mazoezi! Meneja wa Simba Robert Edward amezungumza na Dauda TV na kuthibisha jambo hilo.

Ingawa meneja amekiri Wawa si mchezaji wa kufanya majaribio lakini kuna vitu ambavyo hajijakamilishwa ili beki huyo anaefuga ndevu nyingi aweze kusaini mkataba wa kuichezea Simba.

Post a Comment

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

Previous Post Next Post