Gigy Money Ajutia Kuanika Listi Ya Wanaume Aliotembea Nao


Msanii wa muziki wa Bongo fleva Gift Stanford maarufu kama Gigy Money amefunguka na kuelezea majuto yake kuhusiana na uamuzi wake wa kutaja orodha ya wanaume aliowahi kubanjuka nao.

Kwenye mahojiano na Kipindi cha Kikaangoni cha East Africa Tv, Gigy Money amekiri anajutia kutaja orodha hiyo ya wanaume kwani mpaka leo kuna wanaume wanaogopa kumtongoza kwa kuogopa kuanikwa.

“Kuwataja wanaume nilipitaga nao najutiaga sana, inafanya kuna muda nikose vitu vya maana kwa kuogopa kuwa nitaropoka.

"Kumbe ule ni utoto na ni foolish age kila mtu lazima apitie hata uikimbie ni bora uipitie ukubwani usiirudie. Kwahiyo najutia kuwataja wanaume niliowahi kutembea nao ila sijutii kupitia ile hatua,“amesema Gigy Money.

Mwaka jana Gigy Money alitaja wanaume zaidi ya 10 wengi wakiwa mastaa wa muziki wa Bongo Fleva na watangazaji wa Redio na Tv. 

Post a Comment

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

Previous Post Next Post