Wema Sepetu Afunguka Sababu Iliyomfanya Kutoudhuria Harusi ya Alikiba


Msanii wa Filamu Bongo, Wema Sepetu amefunguka sababu ya kutohudhuria kwenye harusi ya msanii Alikiba. 

Mrembo huyo amesema harusi ya Alikiba iligongana na birthday ya mdogo wake hivyo akashindwa kwenda kwani anaiweka familia yake mbele kwanza. 

“That because ile ni siku ambayo nilimfanyia mdogo wangu birth day party, mdogo wangu alikuwa anatimiza miaka 20 mwaka huu. Kwa hiyo mwaka jana sikumfanyia chochote mwaka huu nikawa nimemuhaidi i will do the party,” amesema. 

“So family first na Alikiba anajua mimi namsapoti mwisho wa siku sina kinyongo chochote namtakia kila la kheri kwenye maisha yake ya ndoa,” Wema ameiambia Bongo5. 

Utakumbuka April 19, 2018 Msanii Alikiba alifunga ndoa na mpenzi wake mjini Mombasa nchini Kenya na April 29, 2018 walifanya sherehe ya pili Dar es Salaam.

Post a Comment

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

Previous Post Next Post