Mapenzi Yamliza Nisha Atamani Kuwa Bachela Ajifariji na Sikomi ya Diamond


Wimbo wa msanii Diamond Platnumz ‘Sikomi’ wamfariji  na kumtoa machozi muigizaji Nisha   baada ya mpenzi huyo kuonekana kupitia kipindi kigumu katika mapenzi  na kutamani kuwa Bachela.

Hivi karibuni kumekuwa na stori kuwa aliyekuwa mpenzi wa Nisha amekwapuliwa na mwanadada Snura Mushi ambaye ndiye anatoka naye kimapenzi.

Hata hivyo muimbaji huyo amekuwa akikanusha hilo kwa kueleza wapo pamoja kikazi tu na si vinginevyo.

Wimbo huo ambao maudhui yake unazungumzia mapenzi kwa mtu ambaye ametendwa, unasikika katika video ambayo ameiposti Nisha katika ukurasa wake wa Instagram ambapo anaonekana akiliakwa uchungu.

Post a Comment

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

Previous Post Next Post