Mke Wangu Kapata Bwana Instagram

 

Habari zenu,

Najuta mke wangu kujua haya masimu ya kufuta futa.Yani mwanzo kwa hela yangu nilimnunulia simu hiyo ya kisasa ili aendane na wenzake akaja akaiuza kwani ilikuwa inajizima na istack akarudi kwenye tochi nikaona afadhali tukakaa miezi kadhaa akawa hana simu.

Sasa dada yake akaja akamnunulia simu pana kubwa hapo ndio balaa ilipoanzia yaani amekuwa mgonjwa wa simu yuko instagram kila saa hadi usiku ni huko huko hakuna cha mapenzi wala nini salama labda iishe charge na umeme uwe umekatika.

Nina siku 14 na zaidi hakuna cha mapenzi wala nini akishapika anaingia kwenye simu,mume wake amekuwa simu hasa instagramu.

Sasa nifanyeje?

Post a Comment

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

Previous Post Next Post