MAJANGA: KONDAKTA AFIA GESTI, MCHEPUKO ATOKA NDUKI...

 

Wannanchi wakiwa wamekusanyika katika mtaa wa mabanda
MWANAMUME mmoja aliyefahamika kwa jina la Benard Mwendwa Musyoka (30), maarufu ‘Boy’ au ‘Swaleh’ amekutwa amefariki duniani katika chumba kulala wageni kwenye mtaa mmoja wa mabanda kaunti ya Nairobi  nchini Kenya. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Kisanga hicho cha kutatanisha, kimethibitishwa na Mkuu wa polisi katika eneo la Makadara, Timon Odingo ambaye amefafanua kuwa tukio hilo limetokea katika mtaa wa mabanda wa Mukuru-Reli katika wadi ya Landi Mawe nchini humo.

Odingo aliongeza kwamba mwishoni mwa wiki Musyoka ambaye ni kondakta wa daladala maarufu kama ‘matatuu’ alifika katika Dreamland Guest House na kukodi chumba cha kulala.

“Mwanamume huyo alikodisha chumba alale kama mteja wa kawaida. Hata hivyo, kesho yake alikuwa mwili ukutwa kitandani huku akiwa tayari ameshafariki,” Odingo alisema.

Post a Comment

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

Previous Post Next Post