Kauli ya Kwanza ya Shilole Toka Achezee Kipigo Kwa Mumewe

Mwanamuziki wa bongo na mfanyabiashara Shilole ameibuka tena baada ya siku chache kuposti  picha zikimuonyesha ameumizwa na mumewe baada ya kupigwa na mumewe leo ameibuka na kuwashukuru wa tanzania  kwa ushirikiano kipindi cha matatizo yake.

Kupitia ukurasa wake wa instagram Shilole aliandika hivi

 Salaam ndugu zangu,
Nimeona upendo, nimeona heshima na kukubalika kwa kiwango cha pekee katika wakati huu wa changamoto niliyokutana nayo.
Nashukuru sana kwa upendo wenu, Nashukuru sana wote walionijulia hali na kuniombea dua.
Kuhusu maendeleo yangu mimi niko sawa, naendelea kupambana. Changamoto ni sehemu ya maisha, haziwezi kunifanya nianguke. Lakini yote hayo sio kwa nguvu zangu, ni Mungu na upendo wa Watanzania wenzangu mnaonitakia mema.
Maisha yanaendelea, tuendelee kuijenga jamii yetu : Jamii itakayokataa kabisa unyanyasaji wa kijinsia.

1 Comments

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

  1. Duuuh noma sana, ila haya mambo bhana ni mara 100 ukae kimya tu mapenzi yao na ugomvi wao hatujui chanzo chake ni kipi tusilaumu bure

    ReplyDelete
Previous Post Next Post