Mwinyi Zahera Ashindwa Kuondoka Kimya kimya...... Aibua Madudu Ndani ya Yanga

Baada ya kuondoshwa kibaruani na uongozi wa Yanga kama Kocha, Mwinyi Zahera amezidi kuibua madudu ndani ya klabu hiyo kwa kutaja baadhi ya changamoto alizokutana nazo.

Moja ya hizo ni kuhusiana na kambi waliyoweka Mwanza kwa ajili ya mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Pyramids kuwa hawakufikia kwenye hotel nzuri.

"Kule Mwanza wakati tunajiandaa kucheza na Pyramids viongozi walituweka kwenye hotel ya kwenye mtaa kama wa Kariakoo.

"Ilinibidi niombe namba ya bosi wa GSM ambaye alikuwa Dubai nikazungumza naye na kumueleza juu ya sehemu tuliyofikia.

Bosi akaniuliza kweli Coach mmefikia hapo? Kesho yake akatusaidia tukahama hotel na kwenda hotel nzuri. Namshukuru sana Boss wa GSM".

Post a Comment

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

Previous Post Next Post