Kinyozi wa Cristiano Ronaldo auawa


Mtengeneza nywele wa nyota Cristiano Ronaldo anayefahamika kwa jina la Ricardo Marques Ferreira amekutwa amefariki dunia siku ya Ijumaa katika chumba cha Hoteli huko nchini Uswisi.

Mwili wa Ricardo ulikutwa na mtu wa usafi katika hoteli hiyo ya biashara iliyopota mjini Zurich, Switzerland huku ukiwa na vidonda vya kuchomwa.

Ricardo ambaye anafahamika zaidi kwa jina la Caju ,amekuwa akiishi mjini Zurich kwa miaka miwili iliyopita na alikuwa akiishi katika hoteli hiyo ambayo amekutwa ameuliwa.

Ricardo alikuwa ni mtengeneza nywele (hair stylist) na mpambaji ambaye amefanya kazi na wanamitindo na waigizaji wa kike wa Ureno, pamoja na nyota wa Juventus Cristiano Ronaldo. Ricardo nae anatokea katika kisiwa cha Madeira,Ureno sehemu ambayo ametokea Cristiano Ronaldo.

Post a Comment

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

Previous Post Next Post