Ahadi ya Zlatan kwa Beckham kama Sweden itaifunga England leo


Kuelekea mchezo wa robo fainali ya michuano ya Kombe la Dunia nchini Urusiunaozikutanisha timu za England na Sweden, staa wa soka wa zamani wa Sweden Zlatan Ibrahimovic ameto ahadi nzito kwa David Beckham ambaye ni nahodha wa zamani wa England.
Zlatan na Beckham wote mataifa yao yanakutana katika mchezo wa robo fainali ya game ya World Cup, hivyo Zlatan kupitia ukurasa wake wa instagram amepost picha yake ya zamani akiwa na Beckham na kumwambia kuwa kama England itaifunga Sweden basi atamnunulia chakula cha jioni kutoka katika mgahawa wowote hapa dunini.
Pia Zlatan amemwambia Beckham na kamaSweden ikiifunga England basi atachagua kitu chochote kutoka IKEA Sverige ambalo ni duka na furniture na gharama zitalipwa na David Beckham, kitu ambacho Beckham alikubali na ku-comment.
“Kama Sweden ataifunga England binafsi nitakuchukua hadi IKEA Sverige na kukununulia chochote unachotaka kwa ajili ya mansion yako mpya Los Angels lakini kama England ikishinda nitataka uje Wembley uangalie game ya England ikicheza ukiwa umevaa  jezi ya England na wakati wa mapumziko u-enjoy kwa kula chips samaki”>>>Beckham

Post a Comment

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

Previous Post Next Post