Lionel Messi, Sergio Aguero na Paulo Dybala kwenye kikosi cha Argentina Kombe la Dunia 2018

 Barcelona forward Lionel Messi


Washambuliaji Lionel Messi, Sergio Aguero, Paulo Dybala na Gonzalo Higuain wamejumushwa katika kikosi cha wachezaji 23 watakaoiwakilisha Argentina kwenye kombe la dunia nchini Urusi
Lakini mfungaji bora zaidi wa ligi ya Serie A mshambuliaji wa Inter Milan Mauro Icardi ameachwa nje.
Aguero anajiunga na wachezaji wengine watano wa Premier League akiwemo wanayecheza pamoja huko Manchester City Nicolas Otamendi.
Argentina wataaza mechi za Kombe Dunia dhidi ya Iceland tarehe 16 Juni kabla ya mechi zingine dhidi ya Croatia na Nigeria katika kundi D.
Nusura watupwe nje ya Kombe la Dunia lakini hat-trick ya mshambuliaji wa Barcelona Messi iliwaokoa wakati wa mechi yao ya mwisho ya kufuzu.

Kikosi kamili cha Argentina

Walinda lango: Sergio Romero (Manchester United), Willy Caballero (Chelsea), Franco Armani (River Plate).
Walinzi: Gabriel Mercado (Sevilla), Federico Fazio (Roma), Nicolas Otamendi (Manchester City), Marcos Rojo (Manchester United), Nicolas Taglafico (Ajax), Javier Mascherano (Hebei Fortune), Marcos Acuna (Sporting Lisbon), Cristian Ansaldi (Torino).
Viungo wa kati : Ever Banega (Sevilla), Lucas Biglia (AC Milan), Angel Di Maria, Giovani Lo Celso (wote wa Paris St-Germain), Manuel Lanzini (West Ham), Cristian Pavon (Boca Juniors), Maximiliano Meza (Independiente), Eduardo Salvio (Benfica).
Washambuliaji: Lionel Messi (Barcelona), Gonzalo Higuain, Paulo Dybala (both Juventus), Sergio Aguero (Manchester City).

Post a Comment

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

Previous Post Next Post