Alikiba leo ametaja jina lake halisi

 

Jina la msanii Ali Kiba limeanza kusikika katika masikio ya walimwengu miaka kadhaa iliyopita alipoingia katika game ya muziki wa Bongo Fleva na wengi walimtambua kwa jina hilo la Alikiba.
Lakini unaambiwa jina la Kiba sio jina la ukoo kama watu wanavyodhani jina hilo limetokana na historia fupi katika familia yake, hii ni baada ya mama yake kuwa na ujauzito wake na rafiki zake kumuita mama ‘Kibanio’  kutokana na kutumia kibanio  kubania nguo zake.
Jina la“Kiba” lilikuwa baada ya Ali kuzaliwa na kukuta mama yake akiitwa mama ‘Kiba’ na ndipo watu walipoanza kufahamu jina la Ali Kiba lakini jina halisi la AliKiba ni Ali Saleh Gentamilan.

Post a Comment

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

Previous Post Next Post