Pamoja na pesa ndefu anaelipwa Sanchez, Man United bado ni klabu tajiri kuliko vyote Duniani

Pamoja na kuanza kutoa kiasi cha £600,000 kila wiki kwa ajili ya nyota wao mpya Alexis Sanchez lakini hii haijawafanya Man United kuyumba kifedha na taarifa zinaonesha bado wako kilele cha klabu tajiri ulimwenguni.

Taarifa ya kifedha kutoka kwa shirika la Deloitte inaonesha kwamba Manchester United wanaongoza orodha ya vilabu tajiri ambapo kwa msimu 2016/2017 Manchester United wametengeneza kiasi cha £676.3m.

United wanakuwa wamewapiku Real Madrid kwa mara ya 10 na sasa Real Madrid wako nafasi ya pili kwani kwa msimu wa mwaka 2016/2017 matajiri hao wa Hispania waliweza kutengeneza pesa kiasi cha £674.6m.

Real Madrid wamekaa kwenye nafasi ya Barcelona na sasa Barca wameenda hadi nafasi ya tatu wakitengeneza kiasi cha £648.3m wakifuatiwa na mabingwa wa ligi ya Bundesliga waliotengeneza £587.8m.

Machester City vinara wa ligi kuu Uingereza wapo nafasi ya tano wakitengeneza mpunga wa £527.7m wakifuatiwa na Arsenal ambao 2016/2017 waliweka kibindoni jumla ya £487.6m.

Matajiri wa jiji la Paris(PSG) wako katika nafasi ya saba wakiwa wametengeneza pesa £486.2m, Chelsea wanafuatiwa na £428m, Liverpool £424.2m na Juventus nafasi ya 10 wanamalizia wakiwa wameingiza kiasi cha £405.7m

Post a Comment

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

Previous Post Next Post