Alexi Sanchez atua Man UTD rasmi


Baada ya siku takribani 10 za mvutano, majadiliano na fununu hatimaye jioni ya leo suala la Alexis Sanchez na Henrikh Mkhitaryan kwenda Manchester United limekamilika.
United wamemtangaza rasmi Sanchez kama mchezaji wao ambapo raia huyo wa Chile atakuwa akiweka £600,000 kila mwisho wa wiki kutoka kwa wababe hao wa jiji la Manchester.
Wakati Sanchez akitangazwa kuwa mchezaji mpya wa United, nyota huyo amesema anafuraha sana kuwa mchezaji wa kwanza kutoka Chile kuichezea klabu kubwa duniani.
Sanchez atakuwa anapokea mshahara wa £350,000 kila wiki huku akipewa kiasi cha £100,000 kila wiki itokanayo na haki za matangazo na pia atapewa bonus nyingine ya £140,000 kila wiki.
Wakati Sanchez akitangazwa na Manchester United hii leo, upande wa pili nako Henrikh Mkhitaryan ametangazwa na Arsenal kama mchezaji wao mpya.
Kwa mshahara wa Alexis sasa anakwenda kuwa mchezaji anayelipwa zaidi katika klabu ya Manchester United akiwa mbele ya Paul Pogba ambaye kwa sasa anapokea £220,000 kwa wiki.
Kwa upande wa Mikh aliyekwenda Arsenal amesema klabu hiyo ndiyo ilikuwa klabu ya ndoto zake na tangu akiwa mtoto mdogo alitamani siku moja kuvaa jezi ya Arsenal.

Post a Comment

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

Previous Post Next Post