Mahakama ya Katiba yalitaka bunge kumshtaki Rais

Mahakama ya Katiba nchini Afrika Kusini imebaini kwamba bunge la nchi hiyo lilishindwa kutimiza wajibu wake kwa kushindwa kumuwajibisha rais wa nchi hiyo Ndg. Jacob Zuma juu ya kesi iliyokuwa ikimkabili ya matumizi mabaya ya fedha za umma.

Uamuzi huo wa Mahakama ya Katiba ukiongozwa na Jaji Chris Jafta nchini humo umeainisha kwamba bunge hilo ni lazima lianze mchakato wa taratibu za kumfungulia mashitaka ingawa haikuwa wazi kwamba mchakato huo utaweza kumuondoa madarakani kwa kupigiwa kura.

Mahakama hiyo ilikuwa ikisikiliza kesi  iliyofunguliwa na kambi ya upinzani ambayo ilitaka bunge la nchi hiyo kuanza mchakato wa kumshitaki Rais Zuma.

Rais Zuma anatuhumiwa kutumia fedha za umma kuendeleza makazi yake binafsi.

Post a Comment

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

Previous Post Next Post