Magoli ya Simba yote mawili yalifungwa na John Bocco dakika ya 52 na dakika ya 56, baada ya ushindi huo, kiungo wa Simba raia wa Rwanda Haruna Niyonzima ambaye alikuwa nje ya uwanja kwa majeruhi alitumia ukurasa wake wa instagram kueleza furaha yake hasa uwezo wa Bocco aliouonesha.
“Alhamudulilah kwa ushindi wa leo na pia ongera sanaa wachezaji wote,kiukweli siku ya leo imekuwa siku nzuri yenye furaha na amani,big up my brother Bocco Mungu azidi kukusimamiya mwanangu.Simba nguvu moja najua wataelewa one day”>>>Niyonzima
Tags
Michezo