Waandamana kupinga Ibada za Waislamu kufanyika hadharani

Takriban wanasiasa 100 wa Ufaransa wameandamana katika barabara za makaazi ya Paris kupinga hatua ya Waislamu kufanya ibada ya maombi hadharani.

Wanasiasa hao waliokuwa wakiimba nyimbo ya taifa hilo waliwaondoa takriban wafuasi 200 wa dini ya Kiislamu waliokuwa wakiomba barabarani katika eneo la Clichy.

Maafisa wa polisi hatahivyo walifanikiwa kuyatawanya makundi hayo mawili.

Wakosoaji wanasema ni makosa kwa wafuasa hao wa dini kutumia eneo la umma ambalo linatumika na watu wa dini tofauti.

Waislamu hao hatahivyo wanasema hawana eneo jingine lolote la kutekeleza ibada yao kwa kuwa baraza la mji huo lilichukua chumba kimoja ambacho walikuwa wakitumia kufanyia ibada mnamo mwezi Machi.
Wanasiasa waliokuwa wakiandamana
Image caption Wanasiasa waliokuwa wakiandamana

Ufaransa ina takriban Waislamu milioni tano ,huku wengi wakiwa magharibi mwa Ulaya.

''Maeneo ya umma hayawezi kuchukuliwa kwa njia hii'' , alisemaValérie Pécresse, rais wa baraza la kijimbo la Paris, ambaye aliongoza maandamano ya siku ya Ijumaa yaliofanywa na madiwani na wabunge kutoka chama cha mrengo wa katikati cha Republicans pamoja na vyama vya UDI.

Post a Comment

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

Previous Post Next Post