Magufuli: Tanzania sio shamba la kuchungia mifugo wa taifa jirani

Rais Magufuli amesema kuwa Tanzania sio shamba la kuchungia mifugo ya taifa jirani
  Rais Magufuli amesema kuwa Tanzania sio shamba la kuchungia mifugo ya taifa jirani
Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli amesisitiza kuwa serikali yake itaendelea kuwakamata mifugo watakaoingia nchini humo kutoka taifa jirani.
Akizungumza katika mkoa wa Kagera ambako ameanza ziara yake ya kikazi Magufuli amesema kwamba Tanzani sio shamba la kuchungia mifugo ya nchi jirani na kwamba ataichukulia mifugo hatua kali za kisheria mifugo yoyote.
Vilevile ameitaka nchi Jirani kuchukua hatua kama hiyo iwapo mifugo ya Tanzania itaingia nchini humo kinyume na sheria.
Tanzania kuwapiga mnada zaidi ya ng'ombe 1000 kutoka Kenya
"Tanzania sio shamba la kuchungia mifugo ya nchi jirani, ndio maana tumeamua kukamata mifugo na kuchukua hatua kwa mujibu wa kisheria, na hata huko kwenye nchi jirani wakishika mifugo ya kutoka Tanzania wachukue hatua za kisheria za nchi hizo" alisisitiza rais Magufuli.
Matamshi hayo ya Magufuli yanajiri wakati ambapo kumekuwa na mgogoro wa mpakani mwa Kenya na Tanzania kuhusu mifugo katika siku za hivi karibuni.
Wafugaji wa Kenya wapata hasara kwa kuingiza ngombe zao Tanzania
Wiki tatu zilizopita serikali ya Tanzania ilizikamata zaidi ya ng'ombe 1000 kutoka Kenya na baadaye mahakama moja nchini humo ikaamuru mifugo hao kupigwa mnada na fedha hizo kutumiwa na serikali iwapo wamiliki wa ng'ombe hizo watashindwa kulipa faini ya shilingi milioni 500 za Tanzania.
Mifugo ya jamii ya Maasai nchini Kenya
Na wiki moja iliopita takriban ng'ombe 4000 kutoka Tanzania zilidaiwa kupatikana katika jamii moja ya Maasai mjini kajiado.
Hivi majuzi hatua ya taifa la Tanzania kuwachoma kuku 6,400 kutoka Kenya wenye thamani ya shilini milioni 12 za Tanzania kwa madai kwamba wangesambaza ugonjwa wa homa ya ndege ilizua hizo tofauti kutoka kwa watetezi wa wanyama .
Afisa mkuu wa maswala ya mifugo nchini Tanzania Obedi Nyasembwa alisema kuwa kuku hao waliingizwa nchini humo kinyume na sheria na kwamba uwpo wao nchini humo ulikuwa hatari kwa ndege wengine.

Post a Comment

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

Previous Post Next Post