
Rais wa Tanzania
John Pombe Magufuli amesisitiza kuwa serikali yake itaendelea kuwakamata
mifugo watakaoingia nchini humo kutoka taifa jirani.
Akizungumza
katika mkoa wa Kagera ambako ameanza ziara yake ya kikazi Magufuli
amesema kwamba Tanzani sio shamba la kuchungia mifugo ya nchi jirani na
kwamba ataichukulia mifugo hatua kali za kisheria mifugo yoyote.Vilevile ameitaka nchi Jirani kuchukua hatua kama hiyo iwapo mifugo ya Tanzania itaingia nchini humo kinyume na sheria.
Matamshi hayo ya Magufuli yanajiri wakati ambapo kumekuwa na mgogoro wa mpakani mwa Kenya na Tanzania kuhusu mifugo katika siku za hivi karibuni.
Hivi majuzi hatua ya taifa la Tanzania kuwachoma kuku 6,400 kutoka Kenya wenye thamani ya shilini milioni 12 za Tanzania kwa madai kwamba wangesambaza ugonjwa wa homa ya ndege ilizua hizo tofauti kutoka kwa watetezi wa wanyama .
Afisa mkuu wa maswala ya mifugo nchini Tanzania Obedi Nyasembwa alisema kuwa kuku hao waliingizwa nchini humo kinyume na sheria na kwamba uwpo wao nchini humo ulikuwa hatari kwa ndege wengine.
Tags
kitaifa