Askari JWTZ Ahukumiwa Kunyongwa Hadi Kufa


Askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kikosi cha 08/691 KJ Chandarua mkoani Ruvuma, Sajenti Batsin Sanga amehukumiwa kunyongwa hadi kufa kwa kosa la kuwaua kwa risasi mtalaka wake na mwanajeshi mwenzake.
Songea. Askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kikosi cha 08/691 KJ Chandarua mkoani Ruvuma, Sajenti Batsin Sanga amehukumiwa kunyongwa hadi kufa kwa kosa la kuwaua kwa risasi mtalaka wake na mwanajeshi mwenzake.

Desemba 27 mwaka 2018 katika lango kuu la kambi hiyo, askari huyo mwenye namba za kijeshi MT81337 akiwa na bunduki aina ya AK47, aliwashambulia kwa risasi Veronica Kayombo na Aaskari mwingine na kusababisha wafe papo hapo.

Ingawa jina la askari aliyeuawa pamoja na Veronica halitajwi kwenye hukumu, ushahidi unaonyesha askari huyo alifyatua risasi 10 kati ya 30 alizokabidhiwa huku miili ya marehemu ikikutwa na majeraha ya risasi kichwani. 

Post a Comment

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

Previous Post Next Post