Amber Lulu Anusurika Kufa Baada ya Kupata Ajali Mbaya

Msanii wa Bongo Fleva na video vixen, Amber Lulu amenusurika kwenye ajali ya gari.

Hitmaker huyo wa ngoma Jini Kisirani amepata ajali akiwa anaelekea kwenye birthday producer Mesen Selekta.

"Wiki hii imekuwa ina misuko sukosana kwangu na Shukuru Mungu kwa yote ilikuwa siku ya jana saa 7 usiku tulikuwa tukielekea kwenye birthday ya Messen tulipata ajali mbaya sana na Shukuru tulitoka salama japo mimi nilibanwa mkono lakini nipo salama," ameeleza Amber Lulu.

Kwa sasa Amber Lulu anafanya vizuri na wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la Vuruga.

Post a Comment

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

Previous Post Next Post