IRENE UWOYA HAKUNA WA KUNINYAKULIA DOGO JANJA


STAA mkali wa filamu Bongo, Irene Uwoya amefunguka kuwa yeye ni mwa­namke anayejiamini kuliko watu wanavyo­dhani na wala hana wasiwasi na mwan­amke yeyote kum­chukulia mumewe, Abdulaziz Chende ‘Dogo Janja’.Uwoya alisema alipoamua kuingia kwenye ndoa na mwanamuz­iki huyo alijua wazi ‘nyakun­yaku’ wapo, la­kini kikubwa anajiamini.

Akasema hata mumewe huyo aende wapi anajua hawezi kuhangaika na wanawake wen­gine kwa sababu yeye ni mwanamke aliyekamilika.

“Mimi sio mwan­amke wa kufuatana na mume nyuma kwa sababu najiamiani kuliko na ninajua wazi hakuna ambaye anaweza kunin­yakulia mume wan­gu. Najiamini kila idara mimi sina wasiwasi wowote,” alisema Uwoya.

Post a Comment

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

Previous Post Next Post