UTANI: Dogo Janja ampa onyo Billnass kwa Uwoya “Michezo yako ile”


Msanii wa Bongofleva Dogo Janja usiku wa May 12 2018 kutumia ukurasa wake wa instagram alipost picha akijiziba mikono usoni na kuandika caption inayosema “Tupo Karibu na Kifo kuliko maisha.. #DuniaTunapita☹️ na baadhi ya watu kuanza kuhisi kama anataka kutoka kazi mpya nini?

Billnass

Baada ya post hiyo msanii mwenzake Billnass aka-comment kwa utani na kuandika “Kajamaa unaonekana unaogopa kutangulia kutuachia shemela 😂😂 acha roho mbaya” halafu Dogo Janja akajibu pia kwa utani kwa kumwambia “@billnass na nikitangulia ole wako wee michezo yako ile wallah nakutokea usiku utakula mikwaju 😂”

Bado haijaeleweka ni nini kimemfanya Dogo Janja aandike Tupo karibu na kifo inawezekana ikawa ni kazi mpya kama watu wanvyohisi au kuna kitu cha ziada? ila nikukumbushe tu Dogo Janja mke wake ni muigizaji Irene Uwoya hivyo katika comment zake za utani alilenga kumpa onyo Billnass kwa Uwoya kutokana na Billnass kuchukua headlines hivi karibu kwa video yake akiwa mapenzini na Nandy.

Post a Comment

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

Previous Post Next Post