MICHEZO Jibu rasmi la Lipuli FC kwa Yanga kuhusu Adam Salamba

Baada ya club ya Dar es Salaam Young Africans kuandamwa na majeruhi katika kikosi chake katika msimu huu wa Ligi Kuu na michuano ya Kombe la shirikisho Afrika CAF, iliamua kuiomba club ya Lipuli FC kuwaazima mchezaji wao Adam Salamba ili wamtumie katika michuano ya CAF.
Yanga baada ya kuandika barua hiyo na kutarajia matumaini ya kumpata mchezaji huyo, May 15 2018 club ya Lipuli FC iliandika barua kuijibu Yanga kuhusiana na maombi hayo na kueleza kuwa wamelikataa ombi hilo kwani wamebaini ni kinyume na kanuni za FIFA, CAF na TFF.

Post a Comment

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

Previous Post Next Post