TOP 10: Mastaa waliowahi kukiri kuwa Messi ni bora kuliko Ronaldo



Kumekuwa kuna ubishani wa muda mrefu katika dunia ya soka kwa kizazi hiki cha leo kuwa kati ya Cristiano Ronaldo wa Real Madrid na Lionel Messi nani ni bora kuliko mwenzake, hii ni mada ambayo imekuwa ngumu kuipatia majibu lakini hii ndio TOP 10 ya mastaa wanaoamini Messi ni bora kuliko Ronaldo.
1- “Kama nitalazimika kuchagua mchezaji mmoja nani bora zaidi ya mwenzake, nitamchagua Messi sababu yupo vizuri katika kutengeneza assist na pasi za mwisho lakini nitakuwa nimempa asilimia 51 kwa 49”-Steven Gerrard
Steven Gerrard
2- “Cristiano Ronaldo amekuwa bora na kufanya vizuri duniani lakini Messi yupo juu yake”>>> Ronaldinho

Ronaldinho
3 “Kwangu mimi mchezaji bora duniani ni Lionel Messi”>>> Rafinha

Rafinha
4- “Ningeweza kutaja majina ya wachezaji wengi lakini katika miaka 10 au 15 sasa, nafikiri Messi amekuwa mchezaji bora katika kipindi chote hicho hakuna mashaka Cristiano Ronaldo ni kama Ronaldo wa Brazil anafunga sana lakini kwangu Messi ni bora”>>> Pele

Pele
5- “Nimefanikiwa kukutana na Messi, Ronaldo na Griezmann na nawaheshimu wote ni kweli hawa wote ni bora duniani na tunaweza kutaja wengine pia lakini Messi anacheza kitimu zaidi ya Ronaldo hiyo ndio sababu ya mimi kumuweka juu”>>> Adil Rami

Adil Rami
6- “Cristiano Ronaldo na Lionel Messi wote ni wachezaji bora duniani lakini Ronaldo hajafikia kiwango cha Lionel Messi”>>> David Beckham
David Beckham
7- “Messi ni bora anajua namna ya kucheza, kufunga na anaweza kuwafanya wachezaji wengine wakacheza vizuri naheshima kwa wachezaji wote lakini naamini Messi yupo level nyingine”>>> Pep Guardiola
Pep Guardiola
8- “Napenda Messi namna anavyocheza kama napewa nafasi ya kuchagua mchezaji mmoja bora basi ni wazi nitamchagua yeye, napenda Messi sababu ni bora lakini hakuna mashaka Ronaldo pia ni mchezaji mzuri”>>> Javier Saviola

Javier Saviola
9- “Kwa mimi ukiniambia nitaje TOP 3 ya wachezaji bora wa muda wote duniani nitasema Messi, Pele na Maradona”>>> Jose Mourinho
10- “Kuchagu mmoja ni ngumu lakini mimi nitamchagua Messi ni mtu kutoka sayari nyingine na hata Ronaldo pia lakini nafikiri Messi amekamilika zaidi”>>> Ronaldo de Lima

Post a Comment

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

Previous Post Next Post