Evra anaweza kurejea England ?



Mlinzi wa kushoto wa zamani wa Manchester United  na Juventus Patrice Evra huenda akarejea nchini England baada ya kuwepo kwa tetesi za kutaka kusajiliwa na klabu ya West Ham United.

Evra ambaye kwasasa ni mchezaji huru baada ya kutimuliwa na klabu ya Marseille kwa kosa la kumpiga shabiki kwa madai ya kumdhalilisha, kitendo ambacho kilipelekea kufungiwa kushiriki mashindano ya Ualya hadi June 2018.
Aidha usajili huo unadaiwa huenda ukakamilika leo ambapo Evra anaruhusiwa kushiriki ligi ya nchi lakini sio michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya na Kombe la UEROPA.
Evra na kocha wa sasa wa West Ham David Moyes  wamewahi kufanya kazi pamoja ndani ya Manchester United msimu wa 2013 - 2014 kabla ya Evra kutua Juventus.

Post a Comment

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

Previous Post Next Post