Wafanyakazi walipwa Matofali badala ya pesa

Wafanyakazi katika kiwanda cha matofali kusini mashariki mwa China wanaokidai kiwanda hicho mishahara yao yenye thamani ya $14,050, wamelipwa matofali, inaripotiwa.

Kwa mujibu wa shirika la habari Xinhua, takriban wafanyakazi 30 wa kiwanda hicho huko Nanchang, katika jimbo la Jiangxi , walikubali kulipwa matofali 290,000 badala ya mshahara wanaodai.

Gazeti la Jiangxi Daily linaripoti kuwa wafanyakazi hao , wote wakiwa ni wahamiaji , wametoka katika eneo la milima la jimbo la Yunnan kuini magharibi, na hawakuwa na namna ili kuishi kwa “kutumia mishumaa na kuwasha kuni moto ili kupunguza baridi “.

Baada ya chama chao cha wafanyakazi kuingilia kati na kwa usadizi wa mahakama, wafanyakazi hao walikubali kupokea matofali hayo kutoka wamiliki wa kiwanda badala ya mshahara wao ambao hawajalipwa.

Xinhua linasema kuwa waajiri wao, ambaye hakutajwa jina katika vyombo vya habari, bado anajaribu kutafakari namna ya kuwalipa, tofuati iliosalia ya Yuan 10,000 wanaodai wafanyakazi hao.

Taarifa hii imezusha mjadala mkubwa katika mitandao ya kijamii China, huku wengi wakielezea wasiwasi wao kuhusu ni kwanini mara kwa mara wafanyakazi wa vijijini wahamiaji ndio hulipwa kidogo kidogo?

Wengine wametania wakisema hali imekuwa mbaya kiasi cha matofali kuonekana kuwana thamani sawana fedha.

Post a Comment

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

Previous Post Next Post