Watu tisa wamefariki baada ya
washambuliaji waliojihami na bunduki walipojariubu kuvamia kanisa moja
kusini mwa Cairo, lakini wakazuiliwa na maafisa, maafisa wanasema.
Mshambuliaji mmoja aliuawa na mshipi wake uliojaa vilipuzi kutibuliwa.
Mpiganaji mwengine alifanikiwa kutoroka.
Huduma za usalama zilitangaza mipango wiki hii ya kulinda sherehe wakati wa mwaka mpya na Krisimasi ya kanisa la Coptic.
Walipanga kupeleka kikosi cha kukabiliana na dharura.
Shambulio hilo la siku ya Ijumaa lilifanyika wakati ambapo maafisa wa polisi waliokuwa wakipiga doria nje ya kanisa hilo walikutana na watu wawili waliowashuku, kulingana na mwandishi wa BBC mjini Cairo Radwa Gamal.
Waliwakaribia watu hao wawili ambao walianza kwa kuwafyatulia risasi polisi hao.
Kuna ripoti kwamba watu kadhaa walijeruhiwa ,wawili vibaya.
Tags
Kimataifa