Zitto Kabwe Ajipanga Kulishtaki Jeshi la Polisi

 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhKOtqA9wBpw9MlaHN9-m_MtilrxOOAqOUYuGWJbLAs0iS83JP0EaPjpCA3zXZjkSzEJSYKte97z_A-82YW9u0XfjcQ3j9WQgpwPyU_ci3F4ec6peLNu_pDPZx-puQ01v7Tb_26eicxnO0/s1600/download+%25287%2529.jpg



Mbunge wa Kigoma mjini Mh. Zitto Kabwe amesema anajipanga kulifunguliwa kesi ya kikatiba jeshi la polisi nchini kutokana na kushikilia simu yake.

Zitto ameeleza kuwa Simu yake inashikiliwa tangu 7/11/2017 alipokamatwa kwa tuhuma za kuvunja sheria ya takwimu pamoja na sheria ya makosa ya mtandao.
“Walisema watahitaji simu hiyo kwa siku 2 tu, nilikwenda polisi KAMATA siku 3 baadaye nikaelezwa kuwa bado wanaendelea na uchunguzi. Nimerudi leo tarehe 20/11/2017, Polisi wanasema bado wanahitaji simu yangu hiyo”, amesema Zitto.
Kiongozi huyo wa chama cha ACT-Wazalendo ameongeza kuwa, “Nimeamua kuwaachia Simu mpaka hapo watakapotosheka lakini wajiandae na kesi ya kikatiba ambayo pia italinda haki za wananchi wengi wanaothirika na matumizi mabaya ya sheria ya Mtandao ( Cybercrime Act )”.



Post a Comment

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

Previous Post Next Post