Kenyatta Kuapishwa Jumanne kwa Muhula wa Pili wa Urais

Kenyatta Kuapishwa Jumanne kwa Muhula wa Pili wa Urais

Rais Kenyatta sasa anatarajia kuapishwa kuwa Rais kwa muhula wa pili baada ya Mahakama ya Juu kufutilia mbali kesi ambazo zilikuwa zinapinga ushindi wake katika uchaguzi wa marudio uliofanyika tarehe 26 Oktoba.

Kifungu 141(1b) cha Katiba ya Kenya kinasema Rais anafaa kuapishwa siku ya saba inayofuata siku ya kutolewa kwa uamuzi wa mahakama wa kuidhinisha uchaguzi iwapo kulikuwa na kesi iliyokuwa imewasilishwa.

Rais kwa mujibu wa katiba anafaa kuapishwa hadharani mbele ya Jjai Mkuu au Naibu Jaji Mkuu.

Post a Comment

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

Previous Post Next Post