Dogo Aslay Hizi Sasa Sifa Zimezidi Kipimo..Umetuzalilisha Wanawake



https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEimFo1tn4s5_uCJHJrBnRVRKEfK7CNc1Ugkpa01jMDIjEwcdowO6FmTpKKoz0CyoWe_JQERdxmPFiO58Zu8X_1QHAcHWWvBPdn5JPzzIV-mlctGrKrjUiadMUhIdPf2QReA0Y49DESU9CE/s1600/daogo.webp

Mimi binafsi ni shabiki mkubwa wa nyimbo za dogo aslay ukweli ni kwamba dogo anajitahidi ila kilonifanya niandike hii thread kuna wimbo wa Aslay umetoka sijui kautoa mwenyewe au umevuja au vipi maana wimbo wenyewe una verse moja tu lakini mashairi ya wimbo huo hayajawafurahisha wanawake wengi ikiwemo Mimi.

Ni wimbo ambao unamdhalilisha mwanamke huyu dogo anapaswa atambue kwamba mashabiki wa mziki wake wengi ni wanawake hata kama umeachana na mwanamke huwezi kumtolea matusi kama ya kwenye wimbo wa aslay so aslay kama umo humu Jf acha kudhalilisha wanawake ambao ndo mashabiki zako wakubwa including Ray 4 real.

Baadhi ya mashairi katika huo wimbo;

Kiuno kizito kama engine ya fuso ,
Hauna lolote kitandani yaani upopo,
Unashindwa hata kufua vichupi vyako,
Unanuka jasho makwapani kama choo cha soko..

Hayo ni baadhi ya mashairi kwa kweli hayajatufurahisha wanawake na ni udhalilishaji

So aslay  metudisappoint 90% ya wanawake Tz.
Yangu ni hayo sema nimeshindwa kuapload hiyo audio.

Post a Comment

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

Previous Post Next Post