Jeshi la Polisi linakabiliwa na changamoto mbalimbali.
Kukosa ushirikiano kutoka kwa wananchi, malalamiko ya wapinzani,
ujambazi, mauaji mkoani Pwani, rushwa, raia kujichukulia sheria mkononi
na tabia za waendesha pikipiki za abiria ni baadhi ya changamoto nyingi
zinazofahamika.
Lakini, Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Simon Sirro amechagua masuala matano tu ya kuanza nayo.
Rushwa, bodaboda kutotii sheria na kujihusisha katika uhalifu,
uchelewaji upelelezi wa kesi, wananchi kuchukua sheria mkononi na mauaji
katika wilaya za Mkuranga, Rufiji na Kibiti ni mambo ambayo IGP Sirro
ameahidi kuanza nayo.
“Kuna kikundi cha watu wachache ambao wanafikiri wanaweza kufanya ule
mkoa usiwe na amani,” alisema Sirro jana katika mkutano wake wa kwanza
na waandishi wa habari tangu aapishwe kuwa mkuu wa chombo hicho cha dola
mwanzoni mwa wiki.
“Lakini niwaambie kwamba siku zote haki lazima itatoa majibu na
niwahakikishie Watanzania kwamba suala la Ikwiriri na Rufiji ni la muda
tu.”
Tags
Usalama
Imetulia hiyo
ReplyDelete