Manchester United wameshinda fainali ya Kombe la Europa kwa kuifunga Ajax Amsterdam kwa mabao 2-0 mjini Stockholm Sweden.
Pogba alifunga goli la kwanza
Magoli ya Paul Pogba na Hendrick Mkhitaryan yameipa
United sio tu Kombe bali pia nafasi ya kucheza Klabu Bingwa Ulaya msimu
ujao.
Mapema kabla ya mchezo huo kuanza, timu hizo mbili zilitoa
heshima zao kwa watu waliopoteza maisha katika shambulio mjini
Manchester. Pia wachezaji wa Manchester United walivaa vitambaa vyeusi
mikononi kama ishara ya heshima kwa waathirika.
Paul Pogba akishangilia bao la kwanza
Wakicheza bila ya mfungaji bora wao Zlatan
Ibrahimovic, pamoja na mabeki Marcos Rojo, na Luke Shaw, pamoja na Erick
Bailly anayetumikia adhabu ya kadi nyekundu, kikosi cha Mourinho
kililazimika kujituma kwenye mchezo huu wa 64 msimu huu.
Wakitumia
uzoefu, pamoja na jinsi walivyojipanga, waliweza kukisumbua kikosi cha
Ajax ambacho kilikuwa na wachezaji chipukizi, wakiwa na wastani wa umri
wa miaka 22. Hendrick Mkhitaryan akishangilia goli la pili na Pogba
Manchester United sasa wanaungana na Chelsea,
Tottenahm na Manchester City katika kucheza Klabu Bingwa Ulaya. Pia
ushindi huu utawaingizia kitita cha takriban pauni milioni 50.
Hili ni kombe la Pili Mourinho anashinda na United katika msimu wake wa kwanza. United walishinda Kombe la Ligi mwezi Februari.