BALOTELLI, SILVA, LENNON, REAL MADRID: TETESI KUBWA ZA SOKA ULAYA LEO JUMATATU

Mshambuliaji wa Marseille Mario Balotelli, 28, anasema kuwa anataka kumaliza kazi yake ya kusakata soka kwa kuichezea timu yake ya nyumbani ya Brescia nchini Itali. (goal)

Mkufunzi wa Everton Marco Silva anasema kuwa anajua kwamba yuko chini ya shinikizo baada ya kikosi chake kushindwa na klabu ya Wolves na kusalia katika nafasi ya tisa katika jedwali la ligi ya Uingereza. (mirror)

Klabu ya Leeds inataka kumnunua winga wake wa zamani Aaron lennon, 31, kurudi katika klabu hiyo kwa kupitia kumsajili kutoka klabu ya Burnley mwisho wa msimu huu. (sun)

Mshambuliaji wa Stoke City Bojan Krkic ,28, huenda akahamia katika klabu ya ligi ya Marekani New England Revolution ambayo imejitolea kumlipa mara mbili marupurupu yake huku dirisha la uhamisho nchini Marekani likiendelea kuwa wazi hadi tarehe mosi mwezi Mei. (sun)

Real Madrid haitamuuza kwa mkopo mwisho wa msimu huu kiungo wa kati wa Uhispania mwenye umri wa miaka 19 kinda Ibrahim Diaz ambaye walimsajili kutoka Manchester City. (AS)

Shirikisho la soka la Uingereza FA linataka kuanzisha refa wa kwanza atakayesimamia mechi za ligi ya wanawake ya.. (telegraph).

Kiungo wa kati wa Newcastle Sean Longstaff, 21, huenda akaitwa na timu ya Uingereza ilio na wachezaji wasiozidi umri wa miaka 21 baada ya kushirikishwa katika kikosi cha kwanza cha timu hiyo.(Chronicle).

Kipa wa Real Madrid Thibaut Courtois angependelea kwamba klabu hiyo ingemsaini mshambuliaji wa Ubelgiji na Chelsea Eden Hazard, 28, badala ya raia wa Brazil na Paris St-Germain Neymar, 26. (Het Nieuwsblad, via Sun on Sunday)

Chelsea huenda ikaipatia upinzani Manchester United kwa kumwania mkufunzi wa Tottenham Mauricio mwisho wa msimu huu . (Sunday Express)

Juventus inataka kumsajili upya kiungo wa kati wa Manchester United Paul Pogba, 25, na kumchezesha raia huyo wa Ufaransa na kiungo wa kati wa Wales Aaron Ramsey . Klabu hiyo ya Itali inatarajiwa kumsajili Ramsey wakati kandarasi yake itakapokamilika msimu huu. (iBancoNero, via Sunday Mirror)

Kutoka BBC

Post a Comment

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

Previous Post Next Post