SIMBA WAKUTANISHWA NA GOR MAHIA FAINAL YA SUPER CUP


Mchezo wa nusu fainali ya pili ya SportPesa Super Cup kati ya Singida Unted dhidi ya Gor Mahia imechezwa leo katika uwanja wa Afraha Nakuru nchini Kenya na kuhudhuriwa na mashabiki mbalimbali.
Gor Mahia wakiwa nyumbani na mashabiki wengi uwanjani, wamefanikiwa kupata ushindi wa magoli 2-0, ushindi huo sasa unaifanya Gor Mahia kuingia fainali ya SportPesa Super Cup na watacheza dhidi ya Simba SC.
Kwa upande wa Singida United wao sasa watacheza mchezo wa kuwania nafasi ya tatu dhidi ya Kakamega Home Boys, ambao wao walitolewa mapema katika mchezo wa nusu fainali ya kwanza dhidi ya Simba SC.

Post a Comment

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

Previous Post Next Post