HUYU HAPA KOCHA MPYA WA MBAO FC


Club ya Mbao FC ya jijini Mwanza baada ya kocha wao mkuu Ettiene kuihama club hiyo na kuamua kujiunga na club ya KMC ya Manispaa ya Kinondoni, leo club hiyo imeamua kumtangaza kocha wao mpya.

Mbao FC mbele ya wadhamini wao wakuu GF Trucks wamemtangaza Amri Said kuwa kocha wao mpya mkuu na ataanza kukinoa kikosi hiko kwa ajili ya msimu mpya wa Ligi Kuu msimu wa 2018/19.

Kama humfahamu Amri Said alikuwa mchezaji wa zamani wa club ya wekundu wa Msimbazi Simba, kabla ya kuamua kustaafu na kuingia rasmi katika kazi ya ukocha wa mchezo wa mpira wa miguu.

 

Post a Comment

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

Previous Post Next Post