Idris Sultan amkingia kifua mke wa Ali Kiba mtandaoni


Leo May 11,2018 staa mkongwe katika game ya Bongo Fleva Ali Kiba amefanya ziara katika kituo cha redio cha Clouds Media akiongelea ishu mbalimbali kuhusiana na maisha mapya  ya ndoa na katika ziara hiyo aliongozana na mke wake Amina.

Baadhi ya mashabiki wamechukilia hii ishu kuwa sio kitu kizuri kwa mwanamke aliyeolewa kufanya ziara katika vyombo vya habari na kuandika comments tofautitofauti kupitia mitandao ya kijamii hasahasa mtandao wa instagram.

Mchekeshaji Idris Sultan ameamua kuwajibu mashabiki wote ambao wanahisi kuwa kitendo cha mke wa Ali Kiba kufanya ziara “AliKibaDay” na mume wake  ni kitendo kibaya .

Post a Comment

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

Previous Post Next Post