Manara Ammwagia Sifa Ajibu "Ajib ni Mzuri Mara Tatu Zaidi ya Samatta"


Mkuu wa kitengo cha mawasiliano katika klabu ya Simba, Haji Manara amesema kwamba mchezaji wa timu ya Yanga Ibrahimu Ajib ni mzuri lakini hapendi kufanya mazoezi na pia kubaki katika kiwango bora kwa muda mrefu. 

Manara amezungumza hayo  April 18, katika kipindi cha KIKAANGONI  kinachorushwa mubashara kupitia kurasa za kijamii ya EATV na kuongeza kwamba licha ya kipaji alichonacho lakini anashindwa kukilinda kwa kufanya juhudi mazoezini 

“Ibrahim  Ajib anaanza vizuri msimu halafu ikifika mahali akishakua Mfalme katika timu anapumzika, halafu Ajib hapendi mazoezi, hawezi kucheza mechi saba mfululizo katika kiwango cha juu kwasababu hapendi mazoezi , kama angependa mazoezi ni mzuri mara tatu zaidi ya Mbwana Samatta”, alisema Manara 

Kwa upande mwingine Manara amesisitiza kwamba Ibrahim Ajib ni mchezaji mwenye nidhamu ukilinganisha na wachezaji wengine waliotoka timu ya Simba na kuhamia kwa wapinzani wao Yanga.

Post a Comment

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

Previous Post Next Post