"Shahidi Bingwa'
Mkenya mmoja amewashangaza weni kwa siku nyingi baada ya kuto shuhuda ya ajali mbili zilizotokea katika maeneo tofauti nchini humo.Picha ya mwanaume huyo alipotokea kwenye vyombo vya habari zilisambazwa sana katika mitandao ya jamii.
Mwanaume huyo aliyejitambulisha kama Dennis Muigai alihojiwa na kituo ch habari, Citizen TV baada ya ajali ya helikopta iliyowaua watu watano, tarehe 21 mwezi Oktoba.
Na kwa mara nyingine akawashahidi mkuu wakati ajali nyingine iliyotokea mwezi Novemba tarehe 7,huko Murang'a katikati mwa nchi. Ajali hio ilikuwa kilomita 200 kutoka ajali ya kwanza, ambapo gavana wa wa Nyeri alifariki.
Aliwaambia kituo cha televisheni, NTV, kuwa alikuwa abiria kwenye gari la polisi wakati ajali hio ilipotokea na akaelezea yaliyotokea kwa undani.
Kwa mujibu ya vyombo vya habari vya Kenya, baadaye polisi walikamata kwa shutuma za kumuiga afisa wa polisi,haujulikani nini ilimtokea baada ya hapo.
Baada ya yeye kuonekana televisheni, akageuka kuwa mada ya utani, na Wakenya wakaanza mada ya '#WitnessChallenge' kumuiga jinsi ambavyo alivyokuwa pamoja na miwani yake:
Tags
Afrika