Kenya Waanza Kupiga Kura, Wadamka Usiku wa Manane


Wananchi nchini Kenya wameanza kupiga kura katika Uchaguzi Mkuu, wengi wakiwa wamewasili kwenye vituo vya kupigia kura usiku wa manane.

Kwenye kituo cha Shule ya Msingi Mutomo ambako Rais Uhuru Kenyatta atapiga kura watu wamefika hapo tangu saa kumi alfajiri.                      

Pia, kwenye kituo hicho cha Mutomo watu walikuwa wanafanya maombi huku wakiwashirikisha maofisa wa Tume ya Uchaguzi isiyokuwa na mipaka (IEBC) wa kituo hicho kuombea uchaguzi wa amani.                      

Kwenye kituo cha kupiga kura kilichopo Embakasi Social Hall kwenye jimbo la Embakasi East watu walikuwapo hapo tangu saa tisa usiku na kwa mujibu wa mwandishi wetu aliyeko Kenya Noor Shija anasema  foleni hiyo  ilikuwa ndefu umbali wa kiasi cha kilomita tatu.                      

Maeneo mengine ambayo watu wameamka  usiku  ni Mombasa, Naivasha na  Nairobi kwenye kituo cha Shule ya Msingi Kahawa ambako tangu saa kumi Watu wamejazana wakati muda wa kufungua vituo ni saa kumi na mbili.                      

Maeneo mengine imeelezwa vijana walikuwa wakizunguka mitaani wakipuliza mavuvuzela kuamsha watu wakapige kura.                      

Kwa upande wa Nasa  ratiba ya upigaji kura kwa wagombea wao ambapo Raila Odinga atapiga kura   Shule ya Msingi Olympic saa nne na nusu asubuhi                      

Kalonzo Musyoka atapiga kura Shule ya Msingi Tseikuru saa nne asubuhi                      

Musalia Mudavadi atapiga kura kituo cha Shule ya Msingi Chemakanga saa tatu asubuhi

Post a Comment

Kwa maoni na ushauri weka comment yako hapo chini:

Previous Post Next Post